NEWS

MTU WA MALENGO



                                                                     MTU WA MALENGO


Lengo ni shabaha ya kufanya jambo fulani, au ni kusudio la kufanya kitu fulani,au wazo fulani linalokupeleka mahali fulani.
 mtu wa malengo ni mtu anayefanya kitu kwa shabaha.
Binadamu ni kiumbe cha malengo, ili ujitofautishe na wanyama ni lazima uwe kiumbe cha malengo, ukikosa malengo wewe ni sawa sawa na mnyama tu ndivyo Mungu anavyokuona na ndivyo ulivyo.
Mithali 18:3
Mkabithi Bwana kazi zako,
Na mawazo yako yatathibitika.
Mawazo ni makudio, mawazo ni malengo, mawazo ni shabaha, mawazo ni mipango, kila jambo analolifanya mtu linaanzia kwenye mawazo liwe jambo baya au jema.
Kazi yetu ni kuwaza, kazi ya Mungu ni kudhibitisha mawazo yetu, ukikosa malengo utakuwa sawasawa na mwindaji anapiga ndege bila kupima kwanza, malengo ndiyo kipimo chako.

KWANINI TUWEKE MALENGO.
1.       Malengo ni kipimo cha utendaji.

Tunapimautendaji kwa kuweka malengo, ni sawa sawa na mwanafunzi aliyeweka malengo yakupata A, anajipima kwa kupitia lengo halafu akapata B maana yake amefeli kwasababu hajapata A aliyoilenga, au mtu anayefanya buashara katika bidii yake yote alipanga apate 10000 kwa kila siku siku akipata 5000 kwa siku atajua amefeli, malengo ndiyo kitu cha kulinganisha.                                                                                                                                     
2.       Malengo yanakuonesha mwisho wa safari yako.

Huwezi ukajua mwisho wa safari yako kama huna malengo, mtu asiyekuwa na malengo ni sawa na mtu ambaye anasafiri ila hajui mwisho wa safari yake, hata magari yanayosafirisha abilia yanaandikwa Mbeya hadi Dar -es –salam, mtu akifika Iringa anajua kwamba bado hajafika, akifika Morogoro anajua bado hajafika, asiye na malengo anaweza akashuka hata mahali siyo mwisho wa safari yake. Siku moja nilimwuliza mtoto wa shule nilipokuwa nikifundisha somohili kanisani nikamwambia ukimaliza shule unataka kuja kuwa nani? Akaniambia nataka kujakuwa Rubani, anasoma ila anajua mwisho wa safari yangu ni kuwa Rubani, unafanya biashara mwisho wa safari yako ni kuwa nani?, unasoma mwisho wa safari yako ya kisomo ni kuwa nani, kama hujajua utakatisha masoma, au utasoma kupita kiasi.
3.       Malengo yanakupa kutunza muda{ Yanaokoa muda}

Katika vitu ambavyo watu wamefeli, nikutokutunza muda, na sababu ni kukosa malengo, ukikosa malengo utashindwa kutunza muda,ukiwa na malengo muda utakuwa dhahabu kwako, maana kina punzi ya uhai unayoivuta itakuwa ni faida kwako.Zamani walikuwa wanakamata uzululaji, kuna watu leo wao kazi yao ni kuzunguka zunguka kueneza umbeya, ukiwa mtu wa malengo hautofwatilia maisha ya mtu, maana kila dakika unalo la kufanya.
.
4.       Malengo yanaongeza uzalishaji.



Ukiwa mtu wa malengo utaongeza uzalishaji, maana unajua ulikotoka, ulipo na unapokwenda, kwanini wengi kiwango chao chakuzalisha huwa hakiongezeki ni kwasababu si watu wa malengo.Unafanya biashara ila hauongezeki, mtu asiye na malengo ni sawa sawa na kisiwa chenye dhahabu ila bado hakijavumbuliwa, malengo yanakufanya upande viwango siku baada ya siku.
5.       Malengo yanakufanya uwe mtu wa kiasi.


Watu wanaoishi kwakiasi ni watu wamalengo, mtu wa malengo sikuzote ni mtu wa kujizuia, ukiwa mtu wa malengo utachagua, mahali pakuongea, utachagua watu wakushinda nao, utafanya kila kitu mahali pake
1Wakorintho 9:25A
Na kila ashindaye katika michezo hujizuia katika yote.
Ili ushinde katika maisha ni lazma ujifunze kujizuia, ili uishi maisha ya ushindi ni lazima ujifunze kuwa na kiasi, na hauwezi ukawa na kiasi kama huna malengo, malengo pekee yanakudabisha ili uishi maisha ya ushindi
2Timotheo 1:7
Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu naya upendo nay a moyo wa kiasi.
Mungu ameachilia moyo wa kiasi, moyo wakiasi unakaa kwa mtu mwenye malengo, mtu ambaye anajua anakokwenda, ukijua unakokwenda kunavitu hutovifanya, kuna marafiki hutoongea nao, kuna chakula hutokula, kuna maeneo hutoingia maana ni mtu wa malengo, kila kitu unachokifanya hufanyi kwa bahati mbaya.
6.       Malengo yanakukutanisha na watu sahihi.


Zaburi 1:1
Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki,
Wala hakusimama katika njia yawakosaji,
Wala hakuketi kaika njia ya wakosaji

Ili ukutane na watu sahihi, malengo yanachagua watu muhimu, ambao watafanya lengo lako litimie, mfano mwanafunzi, lengo lake ni kusoma ni lazima akutane na mwalimu, ukiwa mtu wa malengo hautoongea na kila mtu, ila wapo watu maalumu ambao utakutana nao.

Daudi anasema heri mtu asiye kwenda katika shauri la wasio , kumbe hao wasio haki ni watu na ukikosa kuwa mtu wa malengo, utakwenda katika shauri la wasio haki.

Kuna watu leo utawakuta wanashinda toka asubuhi hadi usiku kucheza bao tu, halafu huishia kusema jamani maisha ni magumu sana, kumbe maisha yamekuwa magumu kwasababu ya kukaa mahali penye mizaha. Mungu anataka ubadilike ukianza kuwa mtu wa malengo utabadilika kabisa na kuwa mtu mwingine.

7.       Malengo ni mwongozo wa kazi zako.


Malengo ni mwongozo wa kazi yako, mtu asiyekuwa na malengo ni sawa sawa na ndege isiyokuwa na rubani, ni sawa sawa na gari lisilokuwa na dereva litadondoka tu, umefika mahali kila unachokifanya kinaanguka nikwasababu umekosa malengo, malengo yanakupa uwelekeo uelekee wapi katika safari yako,
8.       Malengo yanakupa stamina yakufanya kazi.


Stamina ni kiu, hamu, au huruka, mtu asiyekuwa na malengo ni sawa sawa na gari iliyokosa mafuta, itaenda kwakusukumwa, unafanya kazi zako lakini ndani hujisikii, kutamani kuendelea ni kwasababu huna stamina, yaani umekosa malengo, mtu asiye na malengo siku zote anafanya vitu kivivu, anakwenda kwa kusukumwa. Ikiwa mwanafunzi ameweka lengo la kupata division 1, kitakachomsukuma ni hilo lengo lakupata division 1, au mwingine hana lengo lolote, atakuwa analala hata muda wakusoma.Malengo ndiyo upako wako wa kiutendaji.
9.       Malengo yanakupa kuweka akiba.



Ukiwa na malengo utaweka akiba, mtu aliyekosa malengo anatumia kupita kiasi, wafanya biashara wengi wanajinyima ili mitaji yao ikue, wanaweka akiba ili siku biashara zikigoma watwae katika akiba zao. Katika maisha kuna nyakati mbili kuna nyakati za kupata na kunanyakati za kukosa, ili usiwe masikini, ombaomba katika nyakati za kukosa inategemeana uliweka akiba siku za kupata, akiba si sawa sawa mvua ambayo haitumiki inasubiri kipindi ambacho watu wanapanda ili inyeshe, akiba ni ndugu yako siku ya taabu, ukiwa mgonjwa atakutibu, ukifiwa atakuja kukuona, ukitukanwa atakufariji. 

Mungu anataka ufike mahali unakuwa mtu wa malengo.
 

MTU WA MALENGO MTU WA MALENGO Reviewed by adam on Februari 01, 2017 Rating: 5

Hakuna maoni:

Inaendeshwa na Blogger.